Usalama wa Kompyuta Archives - Fahamu Hili
Thursday, March 28Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Tag: Usalama wa Kompyuta

Njia 4 za Kujilinda Unapofanya Miamala au Manunuzi Kwenye Mtandao

Njia 4 za Kujilinda Unapofanya Miamala au Manunuzi Kwenye Mtandao

Teknolojia
Kutokana na kukua kwa teknolojia ya habari mawasiliano (TEHAMA), mfumo wa biashara pia umebadilika. Hivi leo ni rahisi kutuma na kupokea pesa, kuuza au hata kununua bidhaa kwa njia ya mtandao. Watu wengi hupenda kufanya manunuzi na mauzo ya bidhaa kwenye mtandao kutokana na urahisi wa upatikanaji wa bidhaa na huduma kupitia mtandao. Pamoja na nafasi hii kubwa ya mtandao katika maswala yanayohusu fedha, zipo changamoto mbalimbali zinazoandamana na miamala na manunuzi ya kwenye mtandao. Fahamu jinsi unavyoweza kujilinda unapofanya miamala au manunuzi mbalimbali kupitia mtandao. 1. Tumia kinga-virusi (antivirus) bora Mtandao wa intanet ni chanzo kikubwa cha virusi na wadukuzi. Hivyo ni vyema ukatumia programu madhubuti kwa ajili ya kukukinga na virusi na wadukuzi mara unapofanya manu...
Mambo 8 ya Kufanya ili Kuwa na Nywila (password) Imara na Salama

Mambo 8 ya Kufanya ili Kuwa na Nywila (password) Imara na Salama

Teknolojia
Katika ulimwengu wa leo nywila au password si jambo geni. Mara kadhaa umeona au kutumia password katika vitu na maendeo kadhaa kama vile benki, simu, kompyuta n.k. Jambo la kushangaza ni jinsi watu wanavyotumia nywila bila kujali umuhimu wake katika eneo husika. Mtazamo wa ujumla juu ya nywila (password) Nywila ni ufunguo wa kufungua na kufunga sehemu husika; hivyo aliye nao ndiye atakayeweza kufungua na kufunga. Nywila ngumu = usalama zaidi; nywila rahisi = uslama kidogo. Mhalifu anaweza kutumia nywila kufanya uhalifu. Hivyo basi ni muhimu kufahamu namna ya kutengeneza nywila imara na salama kwa ajili ya kifaa au akaunti yako. Fuatilia makala hii ili uweze kujifunza mambo kadhaa ya kufanya ili kutengeneza nywila imara. 1. Epuka namba na maneno rahisi Wengi wetu hatu...
Usalama wa Msingi wa Kompyuta: Jinsi ya Kujilinda na Virusi, Wadukuzi na Wezi

Usalama wa Msingi wa Kompyuta: Jinsi ya Kujilinda na Virusi, Wadukuzi na Wezi

Teknolojia
Watu wengi hufikiri kuwa usalama wa kompyuta ni swala gumu lenye changamoto kubwa. Inaweza kuwa hivyo kama hukuchukua hatua sahihi mapema. Katika makala hii utafahamu hatua tano muhimu ambazo zitakuwezesha kujilinda na virusi, wadukuzi na wezi katika kifaa chako cha kielektroniki. 1. Wezesha automatiki sasishi (automatic updates) Programu mbalimbali za kompyuta hutoa masasisho (updates) mara kwa mara ili kuziba mianya mbalimbali hasa ya kiusalama iliyobainika katika matoleo ya awali. Program kama Microsoft Window, Mozilla na Chrome ni baadhi ya programu muhimu zinazohitajika kusasishwa kwa wakati. Hivi leo programu mbalimbali huja na usasishaji wa automatiki lakini watu wengi hupenda kuuzima usasishaji huu bila kuzingatia umuhimu wake wa kiusalama. Hivyo basi, ili kuwa salama zing...