Kilimo Archives - Fahamu Hili
Friday, September 29Maarifa Bila Kikomo
Shadow

Tag: Kilimo

Makosa 15 Ambayo Kila Mjasiriamali Anatakiwa Kuyaepuka

Makosa 15 Ambayo Kila Mjasiriamali Anatakiwa Kuyaepuka

Ujasiriamali
Kuanza biashara kutoka kiwango cha sifuri siyo kazi rahisi. Kama mjasiriamali utakutana na changamoto nyingi. Hili haliwezi kuwa tatizo ikiwa uko tayari kujifunza kutokana na makosa na kufahamu njia za kuyaepuka huko mbeleni. Hivi ndivyo wajasiriamali wengi wanavyojifunza na kukua. Unapokuwa kwenye biashara ni lazima ufahamu makosa ambayo yanaweza kuathiri biashara au uwekezaji wako; ili ujitahidi kuyaepuka ama kuyapunguza kadri iwezekanavyo. Ni dhahiri kuwa wajasiriamali wengi wamekwama kutokana na kupuuzia au kutofahamu makosa haya 15 ambayo hata wewe unatakiwa kuyafahamu na kuyaepuka. 1.Kujifanya unafahamu kila kitu Usijifanye unajua kila kitu, hasa kama ndiyo umeingia kwenye ulimwengu wa kibiashara. Kwanini? Kwa sababu kuendesha biashara ni kujifunza na kupata uzoefu. Jitahidi ku...
Kilimo cha Kisasa: Kilimo bila Jua, Udongo wala Maji Mengi

Kilimo cha Kisasa: Kilimo bila Jua, Udongo wala Maji Mengi

Teknolojia
Kwa kawaida kilimo kinahitaji maji, urdhi ya kutosha, jua n.k. Lakini hali ni tofauti kwa kampuni ya AeroFarms ambayo imekuja na mawazo tofauti ya kulima mazao mbalimbali bila kutumia udongo, jua wala maji mengi. Kilimo chao hufanyika ndani ya nyumba tena kwenye ghala la zamani; hii ina maana kuwa kilimo hiki kinaweza kufanyika popote bila kuathiriwa na hali ya hewa. Wazo hili lilianzishwa na Ed Harwood, ambaye ni profesa kwenye Chuo cha kilimo cha Cornel aliyetaka kupanda vitu bila kutumia vitu vinavyokuza vitu. Kilimo bila ardhi au udongo AeroFarms wametengeneza vitu kama rafu au shelfu ambavo zina vitambaa maalumu ambavyo mbegu husiwia juu yake badala ya udongo. Mizizi ya mmea husika hujishikiza katika kitambaa hicho kuelekea chini kujipatia virutubisho na maji. Rafu/...