
Mambo 10 ya Kujifunza Kutoka Kwenye Maisha ya Watoto
Ingawa watu wengine huwachukulia watoto kama watu wasiofaa, watoto ni malaika wa kweli wanaoweza kutufundisha jinsi ya kuishi maisha mazuri. Ingawa wakati mwingine hawatambui wanachokuwa wakikifanya, lakini wanatupa nafasi ya kujifunza vitu vingi ambavyo tunavisahau tunapokuwa watu wazima. Kuna sababu ya kwanini watoto wanaitwa zawadi kutoka kwa Mungu. Wanatufundisha kuboresha maisha yetu, kuona vitu vizuri kwenye maisha pamoja na kujaa tabasamu kila siku. Ni wazi kuwa yapo mambo mengi mazuri na yenye manufaa makubwa ambayo kila mtu anaweza kujifunza kutoka kwa watoto; yafahamu mambo hayo sasa.
1. Kuwa na furaha
Maisha ya watoto yamejaa furaha. Mara nyingi utawakuta watoto wakiimba, wakikimbia, wakiruka, wakitaniana kwa furaha bila wasiwasi. Hili limefanya maisha ya utoto kuwa saw...