
Njia 8 za Kutambua Bidhaa Feki au Bandia
Mara nyingi tunanunua vitu na bidhaa mbalimbali bila kuzifahamu au kuzichunguza vyema. Hili limepelekea watu wengi kununua bidhaa zisizofaa kwao au zenye madhara kwenye afya zao. Kutokana na ukosefu wa elimu pamoja na kuishi kwa mazoea, watu wengi hawajui wala hawachunguzi vyema bidhaa wanazozinunua ili kuhakikisha ubora wake. Madhara ya kutumia bidhaa feki au bandia: Matatizo ya kiafya kama vile saratani na ulemavu.
Upotevu wa fedha.
Ajali (Milipuko, shoti ya umeme, n.k).
Huathiri uchumi. Ni wazi kuwa yapo madhara mengi yatokanayo na matumizi ya bidhaa feki. Hivyo ni vyema ukafahamu njia za kubaini bidhaa hizi.
1. Ofa na matangazo yasiyo ya kawaida
Wahenga walisema “Chema chajiuza kibaya chajitembeza”; ni vyema ukawa makini na bidhaa zenye punguzo kubwa la bei ku...