
Misamiati 20 ya Kiswahili Unayoitumia Kimakosa
Ni wazi kuwa watu wengi wamekuwa wakijitahidi kutumia lugha za kigeni kwa
usahihi kuliko Kiswahili. Ni rahisi mtu kuona aibu kufanya makosa katika
lugha kama vile Kiingereza na Kifaransa lakini siyo Kiswahili.
Ni dhahiri kuwa yapo makosa mengi yanayofanywa na wazungumzaji wa lugha ya
Kiswahili kutokana na kutotilia maanani swala la umahiri katika lugha.
Makosa haya yasipotiliwa maanani yanaweza kukufanya uonekane duni katika
uwezo wako wa kutumia lugha.
Yapo makosa mbalimbali ambayo hufanywa na watumiaji wa lugha yakiwemo yale
ya kimsamiati, kimatamshi, kimuundo n.k.
Katika makala hii nitaonyesha misamiati takriban 20 ambayo pengine
unaitumia au inatumiwa vibaya na wazungumzaji wa lugha hasa kutokana na
makosa ya kimsamiati. 1. Lisaa na Masaa
Lisaa na Masaa ni misamiati au...